Popular Post

Home » » Team Rashid Blog: REAL MADRID VS GALATASARY: MOURINHO NA REKODI YA KUTOPOTEZA MECHI BERNABEU DHIDI YA WATOTO WAKE AKINA DROGBA AMBAO WANA REKODI YA KUSHINDA UGENINI MARA TATU MFULULIZO KATIKA UCL

Team Rashid Blog: REAL MADRID VS GALATASARY: MOURINHO NA REKODI YA KUTOPOTEZA MECHI BERNABEU DHIDI YA WATOTO WAKE AKINA DROGBA AMBAO WANA REKODI YA KUSHINDA UGENINI MARA TATU MFULULIZO KATIKA UCL

Joto la pambano la kugombea kucheza nusu fainali ya ligi ya mabingwa wa ulaya ndani ya dimba la Santiago Bernebau linazidi kupamba moto, na Real Madrid wanaingia kwenye mechi hii wakiwa ndio timu iliyocheza robo fainali nyingi kuliko timu zote kwenye historia ya ligi ya mabingwa wa ulaya - wakicheza mara 30, na sasa wapo kwenye pambano la kuweza kucheza nusu fainali yao ya 24 katika historia yao ndani ya Champions league. 

Sio tu Madrid watakuwa wanapewa sapoti ya kutosha kutoka kwa mashabiki wao wanaofikia 80,000 kwenye mechi hii ya kwanza, lakini pia namba zinawapa nafasi Los Blancos: timu hii ikiongozwa na Jose Mourinho imeenda miezi 14 bila kupoteza mechi kwenye dimba lao la nyumbani kwenye michuano ya ulaya. Lakini bado haitakuwa rahisi, Galatasary, wakiwa wanaongoza ligi ya Uturuki wamekuwa na rekodi ya kushinda mechi tatu za ugenini kwenye Champions league.
Share this video :

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2013. Team Rashid Blogspot . - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger