NYOTA namba moja wa
zamani duniani katika mchezo wa gofu, Tiger Woods na bingwa wa michuano
ya olimpiki ya kuteleza kwenye barafu wa Marekani Lindesey Vonn
wametangaza rasmi kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Wawili
hao walitangaza taarifa hizo katika kurasa zao za mtandao wa kijamii wa
Facebook ambapo walituma picha wakiwa pamoja na kumaliza uvumi uliokuwa
umesambaa juu ya mahusiano yao. Woods
amewahi kumuoa mwanamitindo kutoka Sweden Elin Nordegrem lakini
walitalikiana mwaka 2010 baada ya nyota huyo tajiri kukiri kuwa na
mahusiano na wanawake mbalimbali akiwa ndani ya ndoa yao. Woods
mwenye umri wa miaka 37 amekuwa akihangaika kurejea katika kiwango
chake toka kipindi hicho na sasa ameanza kuonyesha dalili za kurejesha
makali yake ambayo yalimfanya atawale mchezo wa gofu kwa muongo mmoja.
0 comments:
Post a Comment